FAIDA 6 ZA KUWA NA WEBSITE KWA AJILI YA BIASHARA
Je
umekua ukisikia tuu swala la kuwa na website lakini hujaelewa kwanini haswa uwe
na website kwa ajili ya biashara au asasi yako isiyo ya kiserikali (NGO)? Au
unayo website lakini haujaona bado faida za kuwa na website ? Basi makala hii
itakupasha faida haswa ya kuwa na
website kwa namna ambayo pengine hujawahi kufikiria.
Hakuna
wakati ambao website ni ya muhimu kama wakati ambapo tupo katika zama za
utandawazi. Yawezekana ukajiona kuwa unachofanya ni kidogo hivyo hauhitaji website
, hata hivyo kuna mengi utakua unakosa kwa kutokujikita katika kuwa na website
kwa biashara au asasi yako.
Kukipa
thamani ufanyacho
Imekua
kawaida watu wengi kuamini kuwa biashara au asasi yenye website basi itakua
makini . Hata hivyo sio tuu website ili mradi website. Unatakiwa uwe na website
ambayo kweli inaonyesha umakini na ubora wa asasi au biashara yako hii
inajumuisha website yenye muonekano mzuri, yenye maelezo yaliyokamilika, yenye
taarifa ambazo kweli.
Kuleta
ushawishi
Unahitaji
website ili kuweza kujenga uaminifu na kuonekana kweli upo serious. Website
yako itakupa nafasi ya kuwaeleza watu kwa umakini na kwa ushawishi kile
unachofanya na kwanini wakutafute wewe.
Tena website itakusaidia kufanya ushawishi huu kwa watu wengi sana kuliko kuwa
tuu na vipeperushi ambavyo utasambaza kwa watu wachache.
Kuelezea
Ufanyacho
Website
hukufanya uwe na nafasi ya kueleza mambo uyafanyacho kwa watu wengi zaidi. Ni
kweli unaweza kuwa na akaunti nyingi za mitandao ya kijamii . Lakini watu wengi
hawatopata kukufahamu vizuri kama sio kupitia kwa website yako ambapo utakua na
kurasa zilizopangiliwa vema kabisa.
Kupatikana
wakati masaa 24 siku 7 za wiki
Ofisi
yako hufungwa , duka lako hufungwa, lakini website yaweza kupatikana masaa 24
siku 7 za wiki. Hivyo kuwa na website ni fursa kwako kuwafaikia walengwa wako
masaa yote kila siku.
Kuwasiliana
na kuwaelimisha wateja
Kwa
kutumia blog itakayoambatana na website yako utaweza kuwapatia wateja wako na
wale wateja watarajiwa Makala ambazo zitawaelimisha na kuwavuta karibu na wewe.
Pia ni nafasi yako ya kuwapa updates kuhusu bidhaa mpya unazotaka kutoa au
mabadiliko mengine ya kiutendaji , kimarketing na sera za biashara au asasi
yako.
Kuwa
na email address binafsi
Website
itakufanya uweze kuwa na email address inayotaja jina la biashara yako.
Haipendezi na haionekani kuwa “professional” pale unapohitajika kutaja email
address yako halafu ukatumia email yenye domain ya makampuni makubwa kama
gmail, yahoo au Hotmail. Kama kampuni yako ni ABC Limited, basi ni vema ukasema
jinalako@abc.com au jinalako@abc.co.tz
Kwa
wewe unayetaka kuwa na website inayokunufaisha tuwasiliane kwa WhatsApp 0745507517tukusaidie.
Au comment kwa hii post.
0 Comments:
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home