Nguvu ya Biashara ya Mtandao katika Kipato
Biashara
ya Mtandao na Nguvu zake Katika Kukuza Kipato
Kama
tulivyoona katika utangulizi hapo juu,biashara ya mtandao inahusisha usambazaji
wa bidhaa au huduma ili kuwafikia watumiaji toka mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Kwa
kiasi kikubwa hii hufanyika kwa njia ya mdomo toka kwa mtu ambaye anatumia
bidhaa au huduma kwenda kwa mwingine. Uaminifu na mahusioano mazuri ndio msingi
wa biashara ya mtandao.
Nguvu
ya Biashara ya Mtandao katika Kipato
Biashara
ya mtandao inatoa nafasi kubwa katika kuanza na kukuza biashara yenye kukupa
faida katika muda mfupi sana.
Zifuatazo
ni baadhi ya faida kubwa za biashara ya mtandao:
Unaweza
kuanza na Mtaji Mdogo: Biashara ya mtandao ndio biashara pekee unayoweza kuanza
kwa mtaji mdogo sana na yenye uwezo wa kukupa faida kubwa katika muda mfupi.
Makampuni mengine unaweza ukaanza hata kwa Tsh 100,000 tu na mengine yana
viwango vya juu zaidi.
Uwezo
wa kupata Faida Katika Muda Mfupi: Unaweza ukapata faida katika mwezi mmoja tu
kulingana na mfumo ambao kampuni inautumia na juhudi unazoweka katika kujenga
timu chini yako. Shida ya wengi katika
biashara hii hasa katika nchi za afrika ni kuwa hatuichukulii kama biashara na
hivyo kuipa umuhimu mdogo sana. Tunafanya kazi kwa muda mfupi sana, wengine
hawaweki hata saa moja katika wiki nzima kitu ambacho kinasababisha kupata
matokeo hasi.
Muda
Mfupi wa Kazi: Katika biashara hii huhtaji kufanya kazi masaa 8 kama katika
ajira. Masaa 2-4 kwa siku yanaweza kukupa matokeo mazuri sana hivyo kutumia
muda uliobaki katika siku kufanya mambo mengine ikiwemo kukaa na familia yako
au kusafiri.
Kutumia
Nguvu ya Watu: Mafanikio katika biashara ya mtandao yanakuja kwa kujenga timu
ya watu wanaotumia bidhaa za kampuni husika. Na kufundisha ,na kuhimiza kila
mmoja katika timu yako kufanya hivyo hivyo kama unavyofanya wewe. Hii
inakufanya usitumie nguvu nyingi sana kupata kipato kama katika kazi nyingine
za kujiajiri ambapo mara nyingi inategemea uwepo na nguvu za mtu mmoja.
Uwezo
wa Kupata Fedha Nyingi: Biashara hii inauwezo wa kukupa kipato kikubwa katika
muda mfupi. Katika muda wa miaka 3-5 uanweza ukapata fedha nyingi sana ambazo
huwezi kuzipata katika kazi ya kuajiriwa au hata ajira binafsi na biashara
ndogo yoyote. Inakupa uwezo wa kupata hata Tsh Bilioni 1 katika muda wa mwaka
mmoja kulingana na kampuni na mfumo unaotumika ka kampuni husika. [Soma namna ya kutengeneza Tsh Bilioni 1.6
kupitia Biashara ya Mtandao Katika Mwaka 1]
Kwa
hiyo kama mtu anataka kukua kiuchumi haraka,biashara ya mtandao ni sehemu
muafaka kufikia malengo yake kwa haraka na kuondokana na umasikini.
Lakini
ni muhimu kutambua kwamba biashara ya mtandao sio njia ya kuwa tajiri kwa
haraka bila ya kufanya kazi. kazi inahitajika hasa katika mwaka wa kwanza
unapojenga biashara.
Nguvu
ya Biashara ya Mtandao na Intaneti Katika Kukuza Masoko
Tumeona
kuwa vyote intaneti na biashara ya mtandao vyote vina nguvu kubwa kwa namna
tofauti.
Nguvu
ya intaneti ipo katika kusambaza habari kwa haraka na urahisi bila kujali
mopaka ya kijiografia na nguvu ya biashara ya mtandao ipo katika kuwezesha
kusambaza bidhaa toka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa gharama ndogo na
kwa ufanisi mkubwa.
Ukijumuisha
vitu hivi viwili yaani intaneti na biashara yamtandao utapata matokeo makubwa
sana katika mauzo ya bidhaa za kampuni husika.
Unapotumia
intanneti kuweza kuwafikia watu wengi juu ya biashara unayofanya unapata wateja
wengi au watu wengi watakaoona fursa yako na katika hao wengi pia baadhi yao
watajiunga na kununua bidhaa toka katika kampuni yako.
Hapa intaneti
inamwezesha mwanamtandao kuweza kuwafikia watu wengi wengi ambao anaweza
kuanzisha mahusioano nao na hatimaye wakfanya biashara. Mfano mtu anaweza
akakutana na mtu mwingine katika mtandao wa kijamii kama facebook au twitter
kisha wakajenga mahusiano na baadae wakafanya biashara.
Ukiangalia hapa hakuna mipaka kwa mtu mmoja ambaye yupo
katika biashara ya mtandao katika kuwafikia watu. Hii ndio nguvu ya kufanya
boahsra ya mtandao katka intaneti.
Namna
za kuwafikia Watu Kupitia Intaneti:
Mitandao
ya Kijamii: Matumizi ya facebook,twitter,instagram,pinterest etc kukutana na kujemga uhusiano nao ambao baadae
wanaweza wakawa wateja katika kampuni yako ya mtandao.
Blogu
na Tovuti: Tovuti na blogu inawezesha taarifa kuwafikia watu duniani kote.
Blogu ni bora zaidi katika kufikisha taarifa nahupendwa sana na watu kutokana
na habari zake kubadirika mara kwa mara
Barua
Pepe: Ukiwa na anuani nyingi za barua pepe unaweza ukatuma matangazo ya fursa
ya biashara yako na kuwafikia watu wengi kwa mara moja. Baadhi yao kati ya hawa
watapenda na kujiunga na fursa yako.
Mikutano
ya Mbali: Badala ya kukutana na watu ana kwa ana katika mikutano sasa hivi
unaweza kufanya mikutano kupitia mtandao wa intaneti hivyo kuondo kiwazo cha
wapi mtu au watu walengwa wapo.
Kupitia
njia zilizotajwa mwanamtandao anaweza kupata wateja wengi kupitia intaneti.
Kampuni
Inayouza Bidhaa Kupitia Mtandao kwa 100% Na namna ya Kujiunga
Makampuni
mengi ya biashara ya mtandao yanajitahidi kutumia intaneti, mfano kwa
kuelimisha watu na hata kuonesha na kuuza bidhaa zao.
Kampuni
ya QNET ni mojawapo ya makampuni machache yanayotumia intaneti kwa 100%.
Kampuni hii inaonesha bidhaa na kuziuza mtandaoni hivyo kuwezesha wanachama
wake kumilki duka la bidhaa na kuzitangaza duniani kote kupitia tovuti ya
kampuni.
Kama
unataka kutumia nguvu ya biashara ya mtandao na intaneti basi pata taarifa
zaidi kuhusu kampuni hii na ujiunge. Pata taarifa zaidi kuhusu QNET na jinsi ya
kujiunga.
[Kwa
maswali kuhusu fursa ya QNET wasiliana nami kupitia Whatsapp: 0745507517 au
SMS/Piga 0745507507 nitakueleza namna ya kufanikiwa katika Biashara ya Mtandao
na Intaneti]
Hitimisho:
Mafanikio
makubwa katika biashara leo yanaweza kupatikana kama utatumia intaneti.
Biashara ya mtandao hali kadharika ni mojawapo ya biashara ambayo kupitia
intaneti inakupa nafasi ya kupata watu wengi watakaonunua bidhaa toka katika
kampuni yako inayotumia biashara ya mtandao.
Kama
wewe upo katika kampuni ya biashara ya mtandao basi anza leo kujenga biashara
yako kupitia intaneti ili uweze kufaidika ma nguvu ya intaneti katika kukuza
biashara na kipato chako.
Kama
umeipenda makala hii juu basi washirikishe na wengine ili wafahamu juu ya Nguvu
ya Biashara ya Mtandao na Intaneti kuweza kujipatia kipato. Kama una mawazo
,hoja au maswali basi tuandikie hapa chini.
Biashara
njema na tukutane katika makala nyingine.
0 Comments:
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home